19 September 2015

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AENDELEA KUPOKEA MISAADA YA VIFAA MBALIMBALI KUSAIDIA SHULE MPYA YA MSINGI KAKUNI MKOANI KATAVI


WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Peter Pinda amepokea Msaada wa Vifaa vya Shule ikiwemo sare, Kompyuta pamoja na vifaa vya Michezo kutoka kampuni ya Huawei na Benki ya NMB.
 
Pinda amepokea misaada hiyo kutoka Kampuni hizo kwa lengo la kuzindua mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Kakuni katika kijiji cha Kibaoni Wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Shule ya Msingi Kakuni iliyopo kijiji cha Kibaoni Mkoani Katavi ni Shule aliyosoma Waziri Mkuu huyo Mhe,Mizengo Pinda.

Mradi huo wa ujenzi unatarajiwa kukarabati madarasa ya Shule hiyo, barabara na Nyumba za Waalimu.

Meneja Uhusiano wa Huawei, Jin Liguo amesema msaada wa Kompyuta kutasaidia kuboresha Taaluma ya Wanafunzi hususani katika masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT).

Naye Afisa Mkuu wa fedha wa Benki amesema wametoa msaada huo kwa Shule alosoma Mhe,Mizengo Pinda ili kusaidia Watoto walio katika Shule hiyo katika Mavazi pamoja na vifaa vya Michezo ikiwemo Kompyuta. 
 
Mwakilishi wa Kampuni ya HUAWEI nchini Tanzania Bw. Jimmy Liguo Jin (kushoto) akimkabidhi Waziri Mkuu  Mhe. Mizengo Pinda sehemu ya msaada wa kompyuta mpakato zilizotolewa na kampuni hiyo kusaidia wanafunzi wa shule mpya ya Msingi ya Kakuni  iliyo katika kijiji cha Kibaoni mkoani Katavi leo jijini Dar es salaam. Shule hiyo ya kisasa imeanzishwa kufuatia  wazo la Wazo la Waziri Mkuu, Mhe.Mizengo Pinda la kuwa na shule Bora na ya kisasa katika kijiji hicho na inajengwa kupitia michango na misaada ya wadau mbalimbali.
 
 

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname