Saa chache baada ya wimbo mpya wa
Roma ‘Viva Roma viva’ kutoka September 9, rapper huyo amedai kuwa
ametishiwa wimbo huo kufungiwa.
Kupitia Instagram, majira ya saa mbili usiku Roma aliandika;
“WANATAKA KUIFUNGIA NYIMBO YANGU!! KISA TU NIMEONGEA UKWELI!!
INANIUMA SANA NATAMANI HATA KULIA NIKIONA UKWELI HAUPEWI NAFASI!!
NIOMBEENI NA MNIKUMBUKE KWENYE SALA ZENU NDUGU ZANGU!! Viva Roma viva”
Bado haijafahamika sababu ya wimbo huo kutaka kufungiwa, na Roma
hakupatikana kwenye simu yake nilipomtafuta kwaajili ya kuzungumza nae
kuhusu swala hilo.
Usikilize hapa kama bado hujausikilizaHizi ni baadhi ya comments za mashabiki wake waliotoa maoni yao kwenye post hiyo;
paul2297:
Siku zote ukweli haupendwi na walanguzi na wezi kama ccm, na
ninakupongez sana we ni miongoni mwa wasanii wanaojielew, hata kama
wakilifungia leo tunashukuru mungu hataa ndege wa angani wameshalidaka
nyimbo yako na wataendelea kuimba ukweli daima
stella_njau:
Usjal kaka tutakuombea watu kama nyiny tunawahtaji sana katika kuleta
ukomboz najua its not easy kwako coz nchi yetu ni kandamiz but God is
dere to protect u from those damb, selfish and lust leaders VIVA ROMA
VIVA FOREVER tuko pa1 bro
oscarhimxelf:
Mimi huwa najiuliza ivi ulichoimba wewe na alichoongea slaa au mambo
ambayo wanayoongea viongozi kwenye majukwaa ya kampeni mbona hayana
tofauti kwann wao huwa hawafungiwi.. mfano juzi slaa akawa anaongea
mpaka habar za maaskofu sijui kupewa hela na data nyingine mbalimbali
ambazo alisema sikuona ile hutuba imefungiwa bali adi leo inatumika kama
kielelezo lkn ww ukiongea kwann waseme ifungiwe …
mikemrossotza:
Hata waufungie kaka mkubwa mzigo tunao wamechelewa
seniorita_tynaalex Roma we ninoma nimeipenda nyimbo yako I salute you dear mpambanaji mwenzangu
galla_bway:
Kila wanachofanya wanachelewa broo ..ucwaze tutasambaza kuhakikisha jamii unaisikia huu wimbo …pamoja
levi_mkushflani:
HAHAHAHA WANAIFUNGIA WAKAT YLTUSHAIDOWNLOAD!? cc tunayo na ujumbe tushaupata
rosewau:
Mi nilijua tu…lazima ifungiwe…so jiandae tu wangu…
shabani_maulidi:
Viva #Roma#viva ukweli unauma wakifungia tutasikiliza hata kwenye simu
bodaboda Bajaj daladala na majumbani kwetu message sent #viva#Roma#viva
eetaamajiko:
Usijal @roma2030 kitaa tushaipata na ujumbe umetufikia, hii
inanikumbusha wimbo wa @nashMc kaka suma walifungia ukwel uliowazi kama
vazi la kahaba,Wenyewe kwenye kampeni zao wanatukana ila hawafungiwi
francy_0903:
Sheria zingine zinavyopitishwa kwa kwel wanabid wàngalie kwa umakin kama
mtu akisema ukwel anfungiwa maana matus ndo yamekatazwa sasa hata ukwel
hawautaki loh tunapoelekea ni pabaya kwa kwel maana hamna wa
kutuongelea juu ya nchi yetu zaid ya sisi wenyewe hawez toka mtu Marekan
aje aongee ukwel juu ya Taifa letu coz hana uchungu kama sie wenyewe
tuliomo ndan ya Taifa,hongera roma wimbo mzur and u r in my prayers

No comments:
Post a Comment