
Rais
mstaafu, Benjamin Mkapa ameponda kauli ya vyama vya upinzani kuwa
vitaleta mabadiliko, akisema kazi hiyo tayari imefanywa na CCM.
Akizungumza
kwenye Uwanja wa Uhuru mjini Bukoba wakati wa uzinduzi wa kampeini za
wagombea wa chama hicho mkoani Kagera, Mkapa alisema chama pekee
kilichobobea katika ukombozi ni CCM na Serikali zake zilizotangulia.
Kiongozi
huyo wa Serikali ya Awamu ya Tatu alisema kuwa lengo la vyama vya
upinzani ni kuing’oa CCM na lengo la chama hicho tawala ni kuendelea
kushika dola, hivyo upinzani unatakiwa kujifunza hadi baada ya miaka 50.
No comments:
Post a Comment