16 September 2015

DR. JOHN POMBE MAGUFULI AMREJESHA NYUMBANI SAID MKUMBA MJINI SIKONGE


1
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dr. John Pombe Magufuli akizungumza huku aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi jimbo la Sikonge Bw. Said Mkumba akionyesha kadi yake ya CHADEMA aliyokabidhiwa na chama hicho kabla ya kurejea CCM akionyesha kadi yake hiyo kabla ya kumkabidhi Dr. Magufuli wakati alipotangaza rasmi kurejea CCM na kukabidhi kadi hiyo kwa Dr. John Pombe Magufuli katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo mjini Sikonge mkoani Tabora.
Dr. Magufuli amewataka viongozi wa CCM wilaya hiyo na mkoa wa Tabora kushirikiana na Ndugu Said Mkumba ili kuhakikisha CCM inapata ushindi wa kishindo katika jimbo hilo, Awali Ndugu Said Mkumba aliuelezea umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo kwamba atazungunguka jimbo zima la Sikonge, Mkoa wa Tabora na ikiwezekana nchi nzima kuhakikisha anaipigia debe CCM ili ishinde kwa kishindo katika uchaguzi wa Rais , Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwaka huu  Oktoba 25 nchini kote.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE SIKONGE)
2
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dr. John Pombe Magufuli na Ndugu Said Mkumba wakimnadi mgombea ubunge jimbo la Sikonge Ndugu George Joseph Kakunda mjini Sikonge leo mara baada ya Said Mkumba kukabidhi kadi hiyo ya CHADEMA na kurejea rasmi CCM huku akiahidi kupiga debe la kufa mtu kwa CCM.
 

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname