
Macho
na masikio ya wengi yanaelekezwa kwa wagombea wawili kutoka vyama vikuu
vya siasa, Dk John Magufuli wa CCM na Edward Lowassa wa Chadema, ambao
uchambuzi wa gazeti hili unaonyesha wana mengi yanayoshabihiana.
Wawili
hao ni kati ya makada saba waliosimamishwa na vyama saba kuwania urais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambao inaelekea kuwa ndiyo
watakaochuana vikali, hasa kutokana na ukweli kuwa Dk Magufuli anatoka
chama tawala na Lowassa, ambaye alikuwa Waziri Mkuu, anaungwa mkono na
vyama vinne vya Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF na NLD vinavyounda Umoja wa
Katiba ya Wananchi (Ukawa).
No comments:
Post a Comment