25 June 2015

Wema Sepetu ahitaji mchango kufanikisha safari yake ya kwenda Bungeni.

Wema Sepetu ni mmoja kati ya wasanii ambao wamejitokeza kuwania nafasi ya Ubunge.

Ili kulifanikisha hili Wema Sepetu ameomba mchango wa hali, mali hata mawazo ili aweze kufikanisha azma yake ya kuingia Bungeni.
Kupitia Instagram Wema Ameandika:

"Uongozi ni utumishi. Naamini kama kijana nina uwezo wa kutumikia vijana wenzangu, mama zangu na nchi yangu kwa ujumla. Hili jukumu langu na letu sote.
Nimeamua kwa dhati kuwatumikia wananchi wa Singida na nchi yangu kwa ujumla endapo nitachaguliwa na chama changu.
Ili nifanikiwe katika hili nahitaji mchango wenu wa mawazo, hali na mali. Najua kila mmoja ana mchango wake katika kulifanikisha hili.
Naomba nitumie nafasi hii kuwaombeni wote michango yenu bila kujali itikadi, jinsia, umri au kigezo chochote. Mchango wako wowote utatusogeza karibu kufikia lengo letu.
Tafadhali kwa anayependa kuchangia anaweza kutuma mchango kupitia namba +255655106538 ambayo imesajiliwa kwa Jina la Ahmed Hashim Ngahemela... Asanteni sana...."


No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname