Mshambuliaji mpya wa Yanga SC
Malimi Busungu leo asubuhi ametupia nyavuni goli mbili wakati timu yake
ikipata ushindi wa goli 3-2 kwenye mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu
dhidi ya Friends Rangers mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa kumbukumbu ya
Karume uliopo maeneo ya Ilala kwenye ofisi za (TFF), Dar es Salaam.
Kpah Sherman alikuwa wakwanza
kuipatia Yanga goli la kwanza akimalizia pasi safi kutoka kwa Busungu na
kuiweka Yanga mbele kwa goli 1-0. Lakini Mussa Juma aliisawazishia
Rangers goli hilo dakika ya 25 ya mchezo.
Busungu aliifungia Yanga bao la
pili akitumia vizuri pasi aliyogongewa na Sherman na kuufanya mchezo huo
kwenda mapumziko huku Yanga wakiwa mbele kwa goli 2-1.
Kipindi cha pili Rangers
walifunga goli la pili kupitia kwa Cosmas Lewis goli hilo likiwa ni la
kusawazisha lakini muda mfupi kabla mchezo haujamalizika, Busungu
alitupia kambani bao la tatu na la ushindi na kuufanya mchezo huo
kumalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa goli 3-2
No comments:
Post a Comment