Moja ya magari ya heshima duniani ni Ranger Rover.
Wachezaji wengi maarufu duniani kote
wanatembelea aina hii ya magari na hupenda kwenda nayo mazoezini.
Ranger Rover ziko za 'Modeli'
tofauti, lakini asikwambie mtu, ni raha na heshima kuendesha aina hii ya gari
mjini.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania,
Mbwana Ally Samatta ame-posti picha kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii
wa Instagram akiwa ameegemea gari ya thamani aina ya Range Rover.
Katika picha hiyo Mbwana ameandika
maneno akieleza kwamba picha haina maelezo mengi kwababu akiyaweka anaweza
kuharibu, lakini akasisitiza kuwa picha inatoa somo kwa wachezaji uzao wa sasa
katika soka la Tanzania.
Stori ya kufurahisha ipo mwishoni
kabisa ambako ameweka maneno haya;
NB: Nishaacha toka 2012 kupiga picha
Kwenye magari ya watu
Tafsiri ya maneno haya ni kwamba toka
mwaka 2012 mpaka sasa, Samatta anapiga picha kwenye magari yake tu. Kwa maana
hiyo Range Rover (pichani chini) ni yake.
Hiyo ilikua ni post
ya Mbwana Samata akiwa mbele ya Range Rover yenye namba ya Tanzania ndani
ya DR Congo.
Sasa hizi ni
taarifa ambazo hauzijui kuhusu Mbwana Samata.
Mbwana ana magari
saba likiwemo Range Rover hilo hapo juu
Vyanzo vyangu vya
habari vimesema kwamba amenunua kwa Tsh milioni 80.
Pia Mbwana ana nyumba
tano hapa Tanzania.
Huu ni mfano wa
kuigwa kabisa na hivi vitu viwe mfano kwa kila kijana mwenye malengo na maisha
yake na sio wachezaji mpira tu. Hakuna cha kukuzuia kufika malengo yako.
No comments:
Post a Comment