Mke wa marehemu Kapteni
John Komba, Salome Komba, amemtaja mrithi wa kiti cha Ubunge Jimbo la
Mbinga Magharibi kuwa ni Cassian Njowoka. Akizungumza na gazeti hili,
mama Komba alisema Njowoka ambaye ni Mkurugenzi wa Chuo cha Ualimu,
Kibamba na Chuo cha Uuguzi Dar es Salaam alikuwa bega kwa bega na mumewe
katika kuwaletea maendeleo.
“Ilikuwa marehemu akiwaza
kusaidia kitu fulani kwa wapiga kura wake, Njowoka alikuwa mstari wa
mbele kuhakikisha wanachangiana kwa hali na mali kufanikisha jambo hilo
kwa wananchi wa Mbinga Magharibi, hivyo anaona anastahili kumrithi,”
alisema mama Komba.
Nao baadhi ya vijana wa
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Jimbo la Mbinga
Magharibi, kwa nyakati tofauti wametaka Njowoka kuchukua fomu ya
kugombea wakati ukiwadia kwani walidai ni kamanda wao wa (UVCCM) Wilaya
ya Nyasa pia ni mlezi wa Umoja wa Wanawake Tanzania wilayani hapo.
Njowoka alipoulizwa na
gazeti hili kama yupo tayari kugombe nafasi hiyo ya Komba, hakukanusha
wala kukubali bali alikiri kupokea maombi hayo kutoka kwa wanachama
wengi wa jimbo hilo.“Natafakari, muda ukiwadia nitaishirikisha familia
na washauri wangu kuona kama niingie au la kwenye kinyang’anyiro hicho,”
alisema Njowoka.
No comments:
Post a Comment