22 April 2015

John Mnyika Amshambulia Zitto Kabwe Mtandaoni, Vita yao Sasa ni zaidi ya Siasa..

Mkurugenzi wa habari na uenezi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amemshambulia kwa maneno makali hasimu wake na adui namba moja wa Chama chake Mhe Zitto Kabwe kwa kumuita muongo na kwamba amewatumia waandishi wa Habari kuandika taarifa za Uzushi kuhusu Mnyika.

Mnyika ametoa tuhuma hizo dhidi ya Zitto asubuhi hii kupitia akaunti yake ya Twitter na kumtahadharisha Zitto kuwa atamchukulia hatua Kali za kisheria kwa kupitosha mazungumzo ya Mnyika na familia ya Mwalimu Nyerere.

Sasa hivi imebainika kuwa ni vita kamili baina ya Zitto na Mnyika hasa baada ya kubainika tetesi kuwa Zitto anagombea jimbo la Ubungo ambalo liko chini ya Mnyika hivi sasa.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname