21 April 2015

DADA YAKE DIAMOND ESMA AFUNGUKA TEAM WEMA WANAVYOMNYANYASA MTANDAONI

Esma mdogo wa Diamond Platnumz, aliyevunja ukimya, asubuhi ya leo juu ya kufuatwa fuatwa na watu wanaodaiwa kuwa ni wa marafiki wa Wema Sepetu #teamWema, ambao wamekuwa wakitukana na kumtaka asimsaidie kaka yake juu ya shughuli zake za muziki.
Na Andrew Chale wa Modewji blog
Kuna misemo mingi juu ya mawifi wengi ‘wanagugu’ hasa wa ndugu wa mme, hilo ndilo lililomkuta dada wa mwanamuziki nyota nayefanya vizuri Bongo nan je ya Bongo, Nasib Abdul ‘Diamond Platnumz’ ajulikanaye kwa jina la Esma maalufu kama ‘Esma Platnumz’ ameamua kufunguka kufuatia kusemwa semwa sana na jamaa wa mmewe, ambao ni kutoka #teamWema.

Esma ambaye ameolewa na Meneja wa msanii Mirror na mfanyakazi wa kampuni ya Wema Sepetu, Endless Fame Films aitwaye Petit Man, ambapo kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Instagram, mapema asubuhi ya leo aliamua kufunguka juu ya wanaomfuatafuata kwa kile anachokiposti hasa kinachohusiana na ‘issue’ za Diamond Platnumz ikiwemo shoo yao ya Mei Mosi mwaka huu, Mlimani City, Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname