22 April 2015

BARUA NZITO KWA DIAMOND,SHAMSA NA WENGINE WENYE MAPENZI KAMA HAYA!!!


Kwenu mastaa wa tasnia mbalimbali Bongo‭, ‬habari zenu bwana‭. ‬Poleni na majukumu ya kila siku ya kulijenga taifa‭.‬
Mkitaka kujua afya yangu‭, ‬mimi ni mzima‭, ‬namshukuru Mungu naendelea kutimiza majukumu yangu‭, ‬likiwemo hili la kuwaandikia barua‭.‬
Nimewakumbuka leo kupitia barua‭, ‬nataka kuwaambia kwamba mimi pamoja na mashabiki wengine wa sanaa yenu tumewachoka‭. ‬Tumechoka kuona na kusikia kila siku mkifanya maigizo kwenye maisha yenu halisi‭.‬
Hivi ni kwa nini kila kukicha tunasikia mnaachana‭? ‬Kwa nini hamdumu kwenye uhusiano wa mapenzi‭? ‬Kwa nini hamdumu kwenye ndoa kama mashabiki wenu wanavyowategemea‭?‬
Penzi linapoanza kushamiri‭, ‬mnalinadi kwenye mitandao na vyombo vya habari‭. ‬Mnawaaminisha mashabiki wenu kuwa mnapendana kwa kauli zenu motomoto lakini ndani ya miezi miwili mitatu penzi chali‭.‬Wengine mnaonesha kwamba mmedhamiria na kuamua kufunga ndoa kabisa‭, ‬lakini kumbe moyoni bado mnakuwa mna lenu jambo‭. ‬Mashabiki wenu wanafurahia kuona mmeoana lakini ndoa nayo haidumu‭, ‬mnaachana‭.‬BOFYA KUISOMA YOTE>>

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname