12 March 2015

Uliona alichoandika Naibu waziri wa fedha mh.Mwigulu Nchemba baada ya kupokea taarifa ya kufutwa uanachama Zitto Z.Kabwe?

kulia ni Mb.Mwigulu Nchemba,katikati ni Mbunge wa Jimbo la Manyovu Kigoma Obama na anaefuata ni Mb.Zitto Z.Kabwe
Imenisikitisha sana,Nimesikia taarifa za kuenguliwa uanachama kwa Mh.Zitto Kabwe ndani ya Chama alichoanzia siasa,alichokitumikia kwa Jasho na mali,alichowekeza muda na akili yake kwa zaidi ya miaka 19.
Zitto amekuwa/anaendelea kuwachachu ya mabadiliko kwa Vitendo kwa Taifa letu.Uwezo wa kisiasa wa Kabwe adhabu yake sio kumfukuza,Demokrasia ni lazima itumike.

Nakusihi kijana Mwenzangu,Mwanasiasa Mwenzangu na Mchumi Mwenzangu kuwa,Taifa linakuhitaji sana wakati huu tunapopambana na ufanyaji kazi kwa mazoea na kuleta "MABADILIKO KWA VITENDO"Hivyo usikate tamaa watanzania watakuhesabia mema kwa yote unayoyafanya kwaajili ya Taifa letu. Mwigulu Nchemba
Chini hapa nimekuwekea twit za Mwigulu Nchemba mara baada ya kupokea taarifa ya kufukuzwa uanachama kwa Zitto Zuberi Kabwe
#Zitto Taifa linakuhitaji,Usikate tamaa

#Zitto Uwezo wako wa kisiasa,adhabu yake sio kuenguliwa.Ww ni hazina kwa Taifa

#Zitto Watanzania wanatambua mchango wako kwa Taifa,Wanakuhitaji usikate tamaa

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname