19 February 2015

PICHA ZA BAADHI YA WAKUU WAPYA WA WILAYA WALIOTEULIWA NA RAIS LEO!!

Mwakalebela kati kati.
Paul Makonda.
Shabaani Kisu wa kwanza kushoto.
Zolothe Steven
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, amefanya uteuzi wa wakuu wapya wa Wilaya, kuwahamisha vituo vya kazi huku wengine wakiachwa.

Habari zilizotufikia hivi punde zinasema majina 27 mapya yameteuliwa huku wengine 11 wakitupwa nje ya uongozi huo.

Walioteuliwa ni pamoja na

1. Katibu Mkuu wa Zamani wa TFF, Freddrick Mwakalebela
2. Mtangazaji wa TBC, Shaban Kisu
3. Katibu wa Hamasa wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Paul Makonda
4. Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mboni Mhita
5. RPC wa zamani, Zolothe Steven.

Majina hayo yametangazwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mjini Dodoma mchana huu.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname