20 February 2015

Davido asema ana maadui wengi ambao wanataka kumshusha kutoka kwenye mafanikio aliyo nayo

Staa wa Nigeria, Davido anaamini kuwa ana maadui tena maadui wengi ambao wanajaribu kumshusha kutoka kwenye mafanikio aliyonayo.

Kupitia Twitter Davido ameandika “I got enemies, I got a lotta enemies Got a lotta people tryna drain me of my energy.”
Hii si mara ya kwanza kwa Davido kulalamika kupitia Twitter juu ya watu ambao hawamtakii kheri, au aliowasaidia na baadae kusahau. Hata hivyo hajamtaja mtu yeyote hivyo haijulikani maadui anaowataja ni kina nani.

Davido anatarajiwa kutumbuiza nchini Kenya March 28.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname