09 February 2015

Ambwene Yesaya ‘AY’ asema kuwa wasanii wengi wa Bongo wanawanufaisha ma producer wa Afrika Kusini kupitia Muziki

STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Ambwene Yesaya ‘AY’ amefunguka kuwa maprodyuza wengi waliopo Afrika Kusini ‘Sauz’ wanapata faida kubwa sana kutoka nchi za Afrika hasa Tanzania kupitia muziki.

Akichonga na Over The Weekend, AY alisema wasanii walio wengi kutoka Bongo wamekubaliana na gharama zao ndiyo maana wanakwenda kurekodi huko kuanzia ‘audio’ mpaka video.

“Sauz sasa hivi imekuwa kama moyo wa muziki kwa Wabongo kutokana na kila mmoja kukimbilia huko kwa sababu tu kuna waandaaji wengi wa muziki. Wanawanufaisha sana, natamani na sisi siku moja Wasauz wakimbilie Bongo kurekodi,” alisema AY.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname