Msanii wa filamu Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ akipozi.
Stori: Gladness Mallya
BAADA ya
hivi karibuni kumwagana na aliyekuwa mpenzi wake wa muda mrefu,
Maximilian Bushoke, msanii wa filamu Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’
amefunguka kwamba hahitaji tena mwanaume kwa sasa.
Akipiga
stori na paparazi wetu, Jini Kabula alisema kutokana na kwamba alikaa
kwenye uhusiano wa kimapenzi muda mrefu na Bushoke na hakuona faida
yoyote, anaujutia muda wake na sasa ameamua kuachana na masuala ya
mapenzi na amejikita kwenye kazi zaidi.
Msanii
wa Bongo fleva, Maximilian Bushoke. “Nimegundua kwamba wanaume ni watu
wanaonipotezea muda tu maana nilimsubiri Bushoke muda wote huo lakini
alivyokuja Bongo akanipotezea hivyo nimeamua kujikita kwenye kazi
zaidi,” alisema Jini Kabula.
No comments:
Post a Comment