Aliyekuwa Mtangazaji wa vipindi vya Michezo wa redio Clouds Dar es Salaam,Ibrahim Masoud 'Maestro' (pichani kushoto) leo amekamilisha usajili wake wa kujiunga na Kituo maarufu hivi sasa cha radio hapa jijini Dar es Salaam cha E FM 93.7.
Maestro
ameungana na magwiji wengine katika utangazaji wa vipindi vya michezo
nchini Maulid Kitenge na Omary Katanga ambao wapo katika radio hiyo
inayokuja kwa kasi jijini.
Pichani Maestro akitambulishwa rasmi na Mkuu wa kipindi cha michezo cha E. sports cha E FM 93.7 Maulid Baraka Kitenge leo.
No comments:
Post a Comment