Mchezaji mmoja wa soka raia wa Cameroon amefariki baada ya kupigwa na
kitu katika kichwa chake kilichorushwa kutoka kwa mashabiki mwishoni mwa
mechi katika ligi ya Algeria.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24 Albert Ebosse aliyekuwa
akiichezea kilabu kubwa ya JS Kabylie alikuwa ameifungia timu yake bao
la pekee katika mechi ambayo timu hiyo ilishindwa kwa mabao mawili kwa
moja na kilabu ya USM Alger.
Kitu kilichomgonga kichwani kilirushwa baada ya
mechi kukamilika,wakati ambapo wachezaji walikuwa wanarudi katika chumba
cha kujianda.
Waziri wa maswala ya ndani nchini Algeria ameagiza kuanzishwa uchunguzi kuhusu mauaji hayo.
No comments:
Post a Comment