10 July 2014

DIAMOND AMLIZA MAMA YAKE


Mama Diamond akilia kwa furaha.
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amefanya tukio la kihistoria kiasi cha kumliza mama yake mzazi, Sanura Kassim ambaye alimwaga machozi kama mtoto mbele za watu.
Tukio la mama Diamond kumwaga machozi lilishuhudiwa na kamera za Amani, juzi Jumatatu, mishale ya saa mbili usiku nyumbani kwake, Sinza jijini Dar es Salaam ambako kulikuwa na ‘bethidei’ ya mama huyo.
SAPRAIZI YA NGUVU
Waalikwa na mama huyo, wote walijua kuwa shughuli ilikuwa ni futari lakini kumbe nyuma ya pazia kulikuwa na tukio la kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mama huyo ambayo inadaiwa alikuwa hakumbuki.
Mmoja wa rafiki wa karibu na familia hiyo, kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini, alisema kuwa hadi jioni, mama Diamond hakuwa akifahamu kuwa aliandaliwa sherehe ya siku yake ya kuzaliwa.

Kilio kikiendelea.

“Mipango yote ilifanywa kwa siri mama Diamond hakujua kilichoendelea. Diamond akiwa Marekani alitoa maelekezo mama yake afanyiwe shughuli hiyo hata kama hayupo kwa sababu siku ya kuzaliwa haijirudii,” alisema rafiki huyo.Soma zaidi hapa>>>>

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname