26 April 2014

TAARIFA MPYA KUHUSU MWANAMKE ALIYECHOMWA KISU KISA MUME WA MTU

Amina Hussein akipata matibabu katika hospital ya taifa Muhimbili.
JESHIla polisi mkoani hapa linamshikilia mwanamke aliyejulikana kwa jina la Pima Mabubu kwa tuhuma za kumchoma kisu mpaka kumjeruhi vibaya mwanamke mwenzake, Amina Hussein akidai ana uhusiano wa kimapenzi na mumewe, Adam Ndekeja, Risasi Jumamosi lina mkasa wote.
 Tukio hilo lililowaacha watu vinywa wazi, lilijiri Aprili 22, mwaka huu shambani katika Kijiji cha Kigwa, Kata ya Ukondamoyo wilayani Uyui, Mkoa wa Tabora.
 KISU KILIVYOFANYA KAZI
Habari kutoka kwa baadhi ya mashuhuda zinasema kuwa, Amina alichomwa kisu mara mbili, kwenye paja mguu wa kushoto kisha kwenye mgongo ambapo kilizama na kutoka mpini tu!
Amina Hussein akikimbizwa hospital baada ya kupatwa na mkasa huo.
 KISA KINASIMULIWA
Kwa mujibu wa taarifa za awali, siku ya tukio, Pima alitoka nyumbani kwake na kumfuatilia mumewe huyo kwenye shamba la tumbaku la kaka wa Amina (jina halikupatikana) ambako alisikia kuwa mwanamke huyo yupo na mumewe.

 “Pima alisikia Amina ana uhusiano na mumewe. Siku hiyo akasikia wapo shambani. Akatoka nyumbani na kufuatilia akijua atawanasa laivu,” kilisema chanzo hicho.SOMA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname