18 January 2014

MBONGO ALIYEKAMATWA MAREKANI KWA KOSA LA KUBAKA BIBI WA MIAKA 62 AACHIWA HURU


Steve Konyagi
Mwaka 2010 kwenye mwezi wa 11 Steve Konyagi Mtanzania anayeishi mji wa Lynn Massachesetts nchini Marekani alishitakiwa na Mtanzania mwenzake (jina kapuni) kwamba amembaka demu wake Mmarekani wakati hua aalikua na miaka 62 na kufikishwa mahakami na kuwa nje kwa dhamana.
Steve Konyagi alikuja Marekani mwezi wa 8 mwaka huo 2010 kabla hata hajakaa sawa akakutana na
balaa hilo la kubaka ambalo kama utapatikana na kosa kifungo chake ni miaka 20 mpaka 40. Steve Konyagi Tanzania anatokea maeneo ya Sinza.
wakati Steve Konyagi alipokua akiendelea na kesi yake ya kubaka bibi Mmarekani wa miaka 62 aliibuka dada mwingine Mtanzania (jina kapuni) aliyewahiishi DMV miaka ya nyuma na kudai nae kabakwa na Steve Konyagi hiyo ilikuwa mwaka 2011. Mahakama iliamua kuondoa dhamana kwa Steve Konyagi na kuMsweka ndani kuanzia wakati huo huku ikiendelea kusikiliza kesi hiyo iliyochukua takriban miaka mitatu.

Vijimambo baada ya kupata tetesi za Steve Konyagi kuwa huru ilinyanyua simu na kumtwangia na yeye bila ajizi alinyanyua na kuanza kuelezea kisa kizima. Vijimambo ilitakakufahamu kulikoni na Steve Konyagi akaanza kwa kusema mwaka 2010 kwenye mwezi 8 aliwasili Marekani baada ya kushinda Creen Card na alifikia kwa dada mmoja anayeitwa Adela ambaye yupo Massachusetts miaka mingi.
Jumamosi moja ya mwezi wa 11, 2010 huyo Mtanzania aliyemshitaki walifika nyumbani kwao akiambatana na demu wake huyo Bibi Mmarekani wa miaka 62 wakati huo sasa hivi huyo bibi atakua na miaka 65. Mara baada ya kufika nyumbani kwao kama ilivyoada ya Steve Konyagi ni mtu wa mchupa sana na baada ya kutembelewa na wageni walianza siku yao kwa kupiga mitungi mpaka usiku mnene na demu wa mshikaji akawa amepagawa na Steve Konyagi mdada akimtia majaribuni mshikaji wake. Baada ya mitungi kukolea Demu wa mshikaji alishindwa kuvumilia alimtonya Steve kwamba kwake yeye hajiwezi na Steve tangia aje Marekani alikua hajaona ndani alikua na kinenge kikali pamoja na hivyo bado alishindwa kula uroda kwa demu wa mshikaji lakini kilichotokea demu kulazimisha sana alichoambulia ni kula pipi kijiti.
 wakati huo mshikaji alikua amezidiwa kwa mchupa alipozinduka alihisi swaiba wake amemtenda kitu mbaya na alipoanza kudodosa demu alijitetea kwa kumsinginzia Steve kwamba amembaka ndipo mshikaji pamoja na kwamba yule demu alikuwa mkubwa kiumri jamaa hakukubali alionelea yaishie mahakamani.
Wakati kesi ikiendelea mahakani huku ikipigwa kalenda Steve Konyagi akakutana na kisanga kingine cha kubaka mwaka uliofuata. Steve Konyagi aliendelea kwa kusema Jumamosi moja ya mwaka 2011 wakati huo nishahama kwa Adela nakaa na mshikaji wangu Mtanzania (jina kapuni) alikuja Demu aliyewahi kuwa girl friend wa mshikaji wangu wakati huu akiwa na jamaa mwingi. Huyu demu ni Mtanzania aliyewahiishi DMV miaka ya nyuma na alizaa na watoto wawili na wanaume wawili tofauti. Kama uanvyojua tulianza kupiga mitungi kama kawaida yangu ilipofika usiku mnene jamaa yangu na huyo bibie waliamua kukumbushiwa penzi lao na mara wakaniacha sebuleni na kuingia chumbani baada ya saa kadhaa yule demu alirudi sebuleni na kunikuta mimi nikiendelea na mitungi na wakati huo alirudi akiwa amejifunga taulo tu akiwa amesalua mpaka kineng'esti chake. Demu alijiunga na club yangu ya mitungi na baada ya muda mchache wote tulijikuta tumesinzia kwenye kochi baada ya kuzidiwa na ulabu.
Baada ya saa kazaa nilizinduka na kujikuta nipo na yule demu wakati huo akiwa bado kalala na huku taulo alilojifunga likiwa limeanguka chini na yeye akiwa kama alivyazaliwa. Baada ya kumuaona na hali ile nilijaribu kumuamsha alipoamka na kujikuta na hali ilie alipiga kelele na kudai nimembaka nilijaribu kujitetea lakini ilishindikana na wakaamua kuita polisi na tangia siku hiyo dhamana yangu ikafutwa na mimi nikaswekwa ndani huku kesi zote mbili kuchanganywa pamoja.
Hatima yangu niliiachia mahakama na wakili wangu kwa hiyo nilikaa ndani mpaka January 13, 2014 nilipoachiwa huru na mahakama kwa kupatikana sina hatia na kilichoniokoa ni DNA walipochukua vipimo vya DNA kwa yule demu wa Kimarakani bibi wa miaka 65 hawakukuta chochote changu kuotoka kwake na walipopima DNA kutoka kwa dada Mtanzania pia waliambulia patupu lakini DNA ilimechi na yule mshikaji wangu aliyewahi kuwa Bwana wake siku za nyuma ambayo siku hiyo ya tukio walivunja amri ya sita.
Kwa hiyo Bwana Vijimambo hiyo ndiyo mchapo wenyewe sasa hivi ni uraiani kama kawaida nachoomba Watanzania wenzangu wawaogope mademu hao yasije yakawakuta yaliyonikuta mimi.
credit : vijimambo blog

SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO 

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname