Mwimbaji
wa muziki wa injili Solomon Mahlangu kutoka nchini Afrka Kusini akiimba
jukwaani jioni hii kwenye uwanja wa Taifa katika tamasha kubwa la
Krismas lililofanyika jijini Dar es salaam likishirikisha waimbaji wengi
kutoka nchi mbalimbali za afrika wakiwemo waimbaji wa Tanzania,
Mwimbaji huyo Nguli wa muziki wa njili ameonyesha uzoefu mkubwa katika
kuimba tofauti na waimbaji wengine waliotangulia ukiacha Ephraim
Sekereti wa Zambia, kutokana na kuimba nyimbo mbalimbali za kizuru
kiingereza na kiswahili kwa ufasaha . kwakweli ilikuwa ni burudani ya
aina yake, lilikuwa ni onesha lililososisimua mashabiki wengi huku
wakishindwa kukalia viti vyao wakati mwimbaji huyo akiwa jukwaani, kila
alilowaamrisha wao walifuata kama zinavyoonekana picha hapo chini kweli
huyu ndiye Solomon Mhlangu.Waimbaji wa mwimbaji Slomon Mahlangu wakiimba jukwaani Mashabiki wakipigishwa saluti na mwimbaji Solomon Mahlangu
Hakuna aliyekuwa amekalia kiti chake wakati mwimbaji huyo akiwa jukwaani akifanya vitu vyake.Hapa ilikuwa kila mmoja akinyanyua kitambaa chake juujuu ili mradi burudani tu.Mashabiki wa Solomon Mhlangu wakiwa ameshikana mikono huku wakiinyanyua juu.Mgeni
rasmi Waziri wa nchi katika ofisi ya waziri mkuu Uratibu wa Sera na
Bunge Mh. William Lukuvi akizungumza katika tamasha hilo na kuwashukuru
waimbaji wa muziki wa injili kwa kuendelea kuhubiri amani nchini lakini
pia akawahakikishia kwamba serikali kitahakikisha amani iliyopo inadumu,
kulia ni mkurugenzi wa Msama Promotion Alex Msama na katikati ni
Ezekiel Maige Mbunge wa jimbo la Msalala hivi
punde atapanda jukwaani mwimbaji nguli wa muziki huo kutoka nchini
Afrika Kusini Solomon Mahlangu ili kuhitimisha tamasha hilo kwa jiji la
Dar es salaam.Mwimbaji
Ephraim Sekereti akitumbuiza kwenye uwanja wa Taifa wakati wa tamasha
la Krismas linaloandaliwa na kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dar es
salaam lillilofany.ka jioni hiiMwimbaji Ephraim Sekereti akifanya vitu vyake jukwaani jioni hii kwenye uwanja wa taifaMgeni rasmi Waziri wa nchi katika ofisi ya waziri mkuu Uratibu wa Sera na Bunge Mh. William Lukuvi akirejea
kukaa mara baada ya kuzungumza na wananchi katika tamasha la Krismas
kulia ni mkurugenzi wa Msama Promotion Alex Msama na na kushoto ni
Ezekiel Maige Mbunge wa jimbo la MsalalaMwimbaji Rose Muhando akiimba na kucheza kwa hisia mbele ya mashabiki wakeMwimbaji Rose Muhando akiimba na kucheza kwa hisia na kundi lake mbele ya mashabiki wakeWaimbaji kutoka kundi la Upendo Kirahilo wakiimba jukwaani.Mwimbaji Upendo Kirahiro akiimba jukwaaniMwimbaji
wa muziki wa injili Boni Mwaiteje akipagawisha mashabiki wake wakati
akitumbuiza kwenye Tamasha la Krismas linaloandaliwa na kampuni ya Msama
Promotion ya jijini Dar es salaam jioni hii kwenye uwanja wa Taifa,
katika tamash hili pia yuko mwimbaji nguli wa muziki huo kutoka nchini
Afrika Kusini Solomon Mahlangu Boni Mwaiteje akionyesha uwezo wa kucheza na masteji shoo wake
No comments:
Post a Comment