BAADA YA PICHA ZA UTATA ZA JUX NA JACK KUZAGAA ZIKIWAONESHA NI WAPENZI, JACK AFUNGUKA NA KUSEMA HAYA...!!
MWANAMITINDO maarufu nchini, Jack Patrick amemtetea msanii Juma
Khalid ‘Jux’ kwa kusema ni marafiki wa kawaida na kukanusha taarifa za
uhusiano wa kimapenzi zilizozagaa.
Jack akiwa na Jux katika pozi.
Alisema anapoona katika mitandao na baadhi ya magazeti yakiandika
kuhusu uhusiano wa kimapenzi, hujisikia vibaya kwa vile kunamtibulia kwa
mpenzi wake anayemhisi vibaya.
“Kama kuna mapenzi lazima ningeweka wazi tu na kama itatokea nitaweka
wazi, naomba watu wasinihukumu kwa kutumia picha, picha ni nyingi na
wataona nyingi zikiendelea kwa sababu sisi wote tunapenda kupiga picha,”
alisema Jack.
Source: GPL
No comments:
Post a Comment