Sura ya mauzo katika sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson
amefunguka kuwa alikwenda Dubai kwa mumewe Sunday Demonte kwa ajili ya
kusaka mtoto kwani kwa sasa hatumii kinga kwa sababu anahitaji kuitwa
mama.
Akistorisha na Ijumaa Wikienda mara tu baada ya kutia maguu kwenye
ardhi ya Jakayaland mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo alilazimika
kurudi mapema kutokana na msiba wa rafiki yake kipenzi aliyemtaja kwa
jina moja la Sofia, Aunt alisema kuwa kwa sasa muda umefika wa kuzaa.
“Hata
mume wangu anatamani sana mtoto, tumekaa na kukubaliana juu ya ishu
hiyo hivyo muda wowote naweza kuwa mjamzito, japo siwezi kuweka wazi
kama ni tayari au bado kuepuka wanga,” alisema Aunt.
Source: GPL
No comments:
Post a Comment