Rapper Webiro Wassira aka Wakazi amefunguka kupitia Bongo5 kuwa kitendo
cha TID kumdiss kuwa haoni wimbo atakoutumbuiza kesho kwenye eviction
show ya Big Brother Africa The Chase kinaonesha kuwa staa huyo wa
‘Kiuno’ hajui anachokiongea.
Jana kupitia Twitter, TID aliandika: Wakazi ataimba wimbo gani, anaenda
kuonyesha kofia zake za marekani#mzee
kasema#radarworththisshit#watuwabaya#msiwemaf**a.
Akijibu kuhusu kile anachoweza kujibu baada ya
tweet hiyo ya TID, Wakazi
amesema: Sasa ntamjibu nini, anaongea vitu asivyovifahamu, yeye hapo
akimuona Wakazi anaona kofia za Marekani sasa mtu kama huyo utaongea
naye!!”
“The greatest ignorance ya mtu ni pale anapoamua kudiss kitu ambacho
hakijui au hajakifahamu bado vizuri , mtu kama huyo huwezi kuanza
kubishana naye, na yeye ananiona mimi Mmarekani, wakati mimi ni
Mtanzania, angekaa miaka mitatu Ulaya au Marekani angejiona na yeye ni
mtu wa huko kwa jinsi upeo wake ulivyo.”
No comments:
Post a Comment