12 February 2016

ETHAD YAFUNGUA SEHEMU YA MAPUMZIKO KATIKA KIWANJA CHA NDEGE CHA KIMATAIFA CHA ABU DHABI




Mnamo Mei mwaka huu, shirika la ndege la la Etihad linategemea kufungua sehemu mpya ya mapumziko katika stesheni ya tatu ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abu Dhabi kwa ajili ya wageni wake wa “Daraja la Kwanza”, wasafiri wenye kadi maalum za Platinum za Etihad, wasafiri wenye kadi maalum za Platinum kutoka washirika wa Etihad na wale watakaotumia huduma ya “Makazi” iliyopo katika ndege zake aina ya Airbus A380. Etihad imewekeza sana katika kutimiza lengo hili kwa ajili ya wageni wake wa hadhi ya juu wanaopenda huduma zenye viwango bora zaidi.
Peter Baumgartner, Afisa Mkuu wa Biashara, alisema: “Huduma hii itakuwa kito katika taji letu hapa Abu Dhabi, ni nafasi nzuri kuonesha umahiri wetu kwenye ubunifu na uvumbuzi. Ni muhimu kwetu kuhakikisha msafiri anapata huduma bora kwanzia uwanjani hadi angani mpaka anaposhuka. Tuna imani huduma na bidhaa tutakazotoa nje ya ndege zitajizolea umaarufu kama za ndani ya ndege na tunategemea wateja watafurahia yote tunayowaandalia.”
Sehemu hii ya mapumziko itapambwa kwa mtindo wa Kiarabu na itaendana na umaridadi na umahiri uliozoeleka na kuhusishwa na jina la Etihad. Sehemu hii itaonesha uzoefu na ustadi wa Etihad na jinsi walivyojikita katika kuleta huduma yenye ukamilifu, kuanzia angani hadi ardhini.

***MWISHO***
Kuhusu Shirika la Ndege la Etihad
Shirika la Ndege la Etihad lilianza shughuli zake mnamo mwaka 2003 na hadi kufikia mwaka 2014, ilikuwa limeshabeba abiria takriban milioni 14.8. Kutoka makao makuu yake huko Abu Dhabi, shirika hili linasafiri au limetangaza mipango ya kuhudumia wasafiri na mizigo kutoka vituo 116 huko Mahariki ya kati, Afrika, Ulaya, Asia, Australia na nchi za Americas. Shirika lina ndege aina ya Airbus na Boeing takriban 120, Zaidi ya ndege 200 zikiwa zimewekea oda, zikiwemo Boeing 787s 66, Boeing 777Xs 25, Airbus A350s 62 na Airbus A380s tano.
Shirika la Etihad pia limewekeza katkia AirBerlin, Air Serbia, Air Seychelles, Alitalia, Jet Airways , Virgin Australia, pamoja na shirika lenye makazi Uswiss Darwin Airline, likifanya biashara kama Etihad Regional. Shirika la Ethihad, sambamba na  airberlin, Air Serbia, Air Seychelles, Alitalia, Etihad Regional, Jet Airways na NIKI, pia hushiriki pamoja nkwatika washirika wa Etihad Airways, brand mpya inayowaleta kwa pamoja mashirika mengine ya ndege yenye uelewa sawa ili kutoa huduma bora zaidi kwa wateja, kuwapa wateja ratiba nzuri Zaidi na kuwazawadia wateja wakudumu.kwa maelezo Zaidi, tafadhali tembelea :www.etihad.com

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname