12 February 2016

BREAKING NEWZZZ......HATIMAYE SERIKALI YAKIFUNGA CHUO CHA TIU

Profesa Yunus Mgaya, Katibu Mtendaji wa TCU

Profesa Yunus Mgaya, Katibu Mtendaji wa TCU
IKIWA ni siku 10 kupita baada ya mtandao huu kuripoti mgomo wa walimu katika Chuo cha Kimataifa cha Tanzania (TIU) kilichopo Kimara Stop-Over, Dar es Salaam, Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imekifutia leseni chuo hicho. Walimu hao waligoma kuingia darasani kwa muda wa mwezi mmoja kutokana na kutolipwa malimbikizo ya mishahara yao pamoja na kutopewa mikataba ya kazi.
Taarifa iliyotolewa na Profesa Yunus Mgaya, Katibu Mtendaji wa TCU kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa, chuo hicho kimefutiwa leseni yake kutokana na kushindwa kutimiza masharti yaliyobainishwa kwenye leseni iliyowepewa.
Mgaya ameleza kuwa, chuo hicho kimeanzisha kufundisha programu za astashahada na stashahada bila ithibati ya mamlaka husika na kuongeza TCU haitambui program zinazotolewa na chuo hicho.
CREDIT: MWANAHALISI ONLINE

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname