11 January 2016

HURUMA....HIVI NDIVYO KAMPENI NA UKAWA VILIVYOMFILISI LOWASSA,WAFANYAKAZI WAKE WALALAMIKIA NJAA KWA KUKOSA MSHAHARA,KAMPUNI KUFUKUZWA PPF


ALIYEKUWA mgombea urais wa CHADEMA, Edward Lowassa imeelezwa kuwa yupo kwenye hali mbaya kifedha na kumfanya ashindwe kulipa pango za ofisi ya Kampuni yake.
Imeelezwa kuwa kiongozi huyo aliyewahi kushika wadhifa wa Waziri Mkuu na kujiuzuru kwa kashfa ya kampuni tata ya kufua umeme ya Richomond, ameshindwa kulipa kodi ya pango ya kampuni inayodaiwa kuimiliki ya Alpha Dry Cleaners iliyopo kwenye jengo la PPF Tower.
Taarifa za ndani kutoka kwenye kampuni hiyo imeeleza kuwa licha ya Lowassa kushindwa kulipa kodi ya pango lakini pia ameshindwa kuwalipa mishahara wafanyakazi wa kampuni hiyo kwa kipindi cha miezi miwili.
Kampuni hiyo ambayo ilikuwa miongoni mwa vyanzo vya mapato vya Lowassa inadaiwa kushindwa kujiendesha kutokana na fedha nyingi kutumika kugharamia kampeni za uchaguzi urais za Lowassa.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari ndani ya kampuni hiyo, kimeeleza kuwa, Alpha Dry Cleaners tangu Novemba mwaka jana, haijalipa kodi kwa PPF.
Hivyo PPF imelazimika kuiandika barua ya notisi ya siku 30 kampuni hiyo kulipa kodi kabla ya hatua zingine hazijachukuliwa ikiwemo kuondolewa kwenye jengo hilo.
Aboubakary Liyongo ambaye ni Msemaji wa Lowassa, Aboubakary Lyongo alisema hawezi kulijua suala hilo kwa kuwa ndio kwanza amelisikia kutoka kwetu na kuomba watafute watu wa Alpha.
“Ndio kwanza nasikia kutoka kwenue kuhusu jambo hilo ila watafuteni watu wa Alpha watakupeni ushirikiano wa kutosha kutoka kwa watu hao,’’alisema.
Hata hivyo, gazeti hili liliwasiliana na Lulu Mengele, ambaye ni Ofisa Habari wa Mfuko wa Pesheni wa Mashirika ya Umma, alisema hayupo ofisini ila atatoa taarifa baada ya kukutana na wahusika.
“Sipo ofisini lakini hiyo nitazungumza na wahusika na watanipa jibu ambalo nitakupa,’’alisema Lulu.
Alpha Dry Cleaners ni moja ya kampuni za Lowassa, ilianza kazi mwaka 1999 ikisimamiwa na Fred Lowassa, ambaye ni mmoja wa watoto wa Lowassa, kabla ya kuanza kwa AlphaTel pale mtaa wa Ohio, ambapo inaelezwa kampuni hiyo ya usafi inachukua tenda ya kufua nguo za wafanyibiashara wakubwa na baadhi ya viongozi wa serikali.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname