22 January 2016

HAYA NDO MAPOKEZI YA RAIS MAGUFULI JIJINI ARUSHA

JO1
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro leo huku akiongozana na Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha Mhe.Daudi Felix Ntibenda tayari kwa hafla ya kuwatunuku kamisheni maafisa wapya wa jeshi la Wananchi waliohitimu vyema mafunzo yao katika chuo cha Jeshi Monduli Mkoani Arusha itakayofanyika Januari 23 /2016. PICHA NA IKULU
JO2
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akishiriki kupiga ngoma za utamaduni wakati alipowasili kwenye uwa nja wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro leo.
JO3
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi waliofika kwenye uwanja wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kumlaki uwanjani hapo.

JO4
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi waliofika kumlaki kwenye uwanja wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro.
JO5
Baadhi ya wananchi wakimpungia mikono Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa KIA mkoani Klimajaro.
JO06
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi waliofika kumlaki uwanja wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro.

JO7
Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ukiondoka kwenye uwanja wa ndege wa KIA kuelekea Arusha mjini

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname