Hali ya kiafya ya Staa na mkongwe wa muziki wa dance Tanzania, Ramadhan Masanjaaka Banza Stone sio nzuri, anaumwa kwa muda mrefu na wapo ambapo waliofikia hatua hata ya kumzushia mitandaoni kwamba amefariki.
Team
ya millardayo.com ilifika nyumbani anapoishi, Sinza Dar es Salaam na
kumkuta pamoja na ndugu zake, alikuwa anaumwa lakini aliongea pia
kinachomsumbua.
Nimeambiwa
kwamba kwa sasa hali yake sio nzuri, imebidi ndugu wampeleke Hospitali
Mwananyamala ili akapate matibabu zaidi.. nina picha pia akiwa
Hospitali, na wapo waliojitokeza kwenda kumjulia hali.
No comments:
Post a Comment