12 January 2016

Gari JIPYA la zaidi ya TSH. MILIONI 200 la MBUNGE mchungaji Msigwa lazua balaa...Wengi washangaa yeye alikataa serikari isiyanunue ila ye kanunua

Peter-Msigwa
Stori: Na Makongoro Oging’, UWAZI
DAR ES SALAAM: Gari la kifahari linalodaiwa kuwa ni la Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa limezua balaa kufuatia mwandishi wetu kumpigia simu ya kutaka kumuuliza swali ambalo lilitoka kwa wapigakura wake kufuatia madai kwamba amelinunua gari hilo kwa shilingi milioni mia mbili.

Jumapili iliyopita, mwandishi wetu alimwendea hewani mbunge huyo na kuanza kwa kumpa hongera kwa kununua gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser V8.
Mchungaji: Nenda kwenye pointi.

2016-Toyota-Land-Cruiser-facelift-front-three-quarter-unofficial-render (1)
Mwandishi: Kuna habari kwamba umenunua gari la kifahari wakati uliwahi ‘kumchana’ aliyekuwa mbunge wa jimbo lako…
Mchungaji: (anafoka) Mbona nyinyi waandishi mnafuatafuata habari za watu? Hamjui kuwa mimi nina vitu vya thamani vingi kuliko hili gari!

Mwandishi: Hapana, hayo ni malalamiko ya wapiga kura wako, wanasema kwamba wewe uliwahi kumsema aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Iringa, Monica Mbega kwamba …
Mchungaji: (anafoka tena) Mnataka kuni-intimidate (kunitisha)? Mimi kuwa na gari hata kama lingekuwa la thamani ya shilingi milioni 500 kuna ajabu gani? Au mnataka kusema nimehongwa na… (anamtaja waziri mmoja wa zamani.)
Mwandishi: Mchungaji unakwenda mbali, haya ni malalamiko ya wapiga kura wako. Ungesikiliza kwanza…
Mchungaji: (anafoka zaidi) Hakuna! Ndiyo maana nyie waandishi wa habari mnakufa masikini. Kazi yenu kufuatafuata maisha ya watu.
Simu inakatika, mchungaji akapiga yeye, mwandishi akampa mhariri wake azungumze…
Mhariri: Mchungaji mbona unazungumza maneno mazito sana?
Mchungaji: (akiwa hajui kwamba sasa anaongea na mhariri wa gazeti) Hakuna, nyinyi hamjui kuwa mke wangu ni mtu mkubwa sana benki ya… (anaitaja jina). Ana uwezo, tena ana mshahara mkubwa kuliko wa wabunge. Nina mashamba makubwa mbona hujanipa hongera? Una uhakika gani kuwa hili ni gari langu?
Mhariri: Ndiyo maana tukakuuliza. Basi kama nimekosea, nisamehe mimi saba mara sabini mchungaji.
Mchungaji: Tena hizo habari mziandike hivyohivyo, wekeni ukurasa wa kwanza kabisa (akakata simu

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname