Bondia
machachari Floyd "Money" Mayweather Jr alitunukiwa mkanda wa (WBO) wa
ubingwa wa dunia katika mchezo wa masumbwi baada ya kumchapa mpinzani
wake raia wa Kifilipino, Manny "Pac-Man" Pacquiao mnamo Mei 2, baada ya
kumshinda kwa ushindi wa pointi.
Lakini
imetangazwa ijumaa ya juzi kuwa bondia huyo mwenye umri wa miaka 38,
atapokonywa mkanda huo kwa kushindwa kutimiza taratibu za umiliki wa
mkanda huo.
Ripoti
zinasema kuwa Mayweather amekataa kulipa kiasi cha dola laki mbili za
kimarekani sawa na zaidi ya milioni 400 za kiTanzania, pili anamili
mikanda miwili ya uzito wa kati yaani WBA na WBC ambapo ni kinyume na
utaratibu wa umiliki wa mkanda huo wa uzito wa juu wa dunia.
Na
imeonekana Mayweather hana cha kujitetea kwakuwa amevunja masharti na
vigezo vya mkanda wa WBO na hivyo atapatiwa bondia mwingine
No comments:
Post a Comment