Staa
wa filamu Bongo, Kajala Masanja. MIEZI michache baada ya Kajala Masanja
kugundulika kuwa na ugonjwa wa uvimbe kwenye kizazi, meneja wa msanii
huyo, Leah Richard amesema hivi sasa yupo sawa kufuatia upasuaji wa
mafanikio aliofanyiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
“Kajala
kwa sasa yupo fiti na tatizo la uzazi limeisha, hivyo mashabiki wake
wasiwe na wasiwasi kabisa kwani atarejea kazini kuendelea kuwapa
burudani,” alisema meneja huyo baada ya simu ya msanii huyo kukosekana
hewani.
No comments:
Post a Comment