11 June 2015

NOMA SANA! KUMBE GARI LA WEMA KIMEO!


Wema akiwa ndani ya gari hilo. Musa mateja
Ni noma! Kumbe lile gari la kifahari aina ya BMW ambalo muigizaji nyota wa filamu Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ alizawadiwa wakati wa bethidei yake na kuwa miongoni mwa sababu za kumwagana na mpenzi wake wa awali, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ mwaka jana, linadaiwa kuwa kimeo kwa vile limekuwa likiharibika mara kwa mara, Amani lina stori kamili.

Gari aina ya BMW la Staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’. Mapema wiki hii, paparazi wetu alikuta gari hilo likiwa limebuma mitaa ya Victoria, Kijitonyama jijini Dar es Salaam huku mshindi huyo wa Shindano la Miss Tanzania mwaka 2006 akiwa ndani, lakini ili kukwepa aibu, aligoma kutoka nje kuomba msaada, badala yake akabakia ndani huku akijaribu kuwasiliana na watu wake wa karibu.  


No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname