Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, amesema hajaweza
kufanya kitu chochote kuwasaidia wasanii kwakuwa wakati anagombea ubunge
hakuna aliyekuwa nyuma yake.
Sugu amelazimika kusema hayo baada ya shabiki kutaka kujua ni kitu gani
alichowafanyia wasanii tangu awe mbunge.
Hao wanaozingua wakamuulize Kikwete studio aliyoitangazia dunia kawapa
wasanii iko wapi na kamkabidhi nani, amehoji Sugu kwenye Instagram. Rais
kashindwa kuwasaidia wanataka kumlaumu mbunge wa Mbeya mjini, wakati
hata hao wasanii wenyewe kimsingi hawakutusapoti kwa namna yoyote wakati
tunagombea huo ubunge, wote walikuwa wanajipendekeza kwenye kampeni za
CCM.
No comments:
Post a Comment