IMEVUJA! Ile mimba ya aliyekuwa Mtangazaji wa Efm Radio, Penieli
Mungilwa ‘Penny’ ambayo ilijulikana alipachikwa na staa wa muziki wa
Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ imezua mzozo upya baada ya kuvuja
kwa madai mengine.
Chanzo makini kimeliambia Amani kwamba, tofauti na madai ya Diamond
kwamba Penny alitoa mimba yake, lakini kumbe Diamond hakumpa mimba ila
ilikuwa ni magumashi ya Penny.
“Hali ilikuwa hivi! Kutokana na
Diamond kutafuta mtoto kwa muda mrefu, hasa kwa mpenzi wake wa nyuma
Wema Sepetu kushindikana, ikabidi Penny atumie mbinu yake ili kufaidika
na pesa za Diamond.
“Penny aliahidiwa na Diamond kwamba, kama
atakubali kuzaa naye atamnunulia gari zuri, kwa hiyo kazi ikawa kwa
Penny sasa, afanyaje?
“Siku moja Penny alimwambia Diamond kwamba amenasa, Diamond akafurahi
sana, lakini kumbe Penny alishaenda kwenye hospitali moja kubwa iliyopo
Kinondoni (jina tunalo), akaongea na nesi mmoja kwamba kama atakwenda
na Diamond kupima mimba akubali kwamba anayo, lengo lake ni kupata
gari,” kilisema chanzo hicho.SOMA ZAIDI>>>
No comments:
Post a Comment