21 October 2014

MAMA ALIYEPIGWA MSHALE WA MAKALIO KISA MAHARI


Ghati Bunyige akiwa amekaa kwenye benchi akisubiri huduma ya matibabu katika kituo cha afya cha Sirari wilayani Tarime mkoani Mara.
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni! Mwanamke mmoja, mkazi wa Kitongoji cha Buriba, Kijiji cha Sirari wilayani Tarime, Mara aitwaye Bunyige Chacha (25) amepigwa mshale kwenye makalio na mumewe, Ghati Nyamarandi kisa kikidaiwa kuanzia kwenye pesa ya mahari na watoto. Akisimulia mkasa wake mzito uliompata Oktoba 5, mwaka huu majira ya jioni, mwanamke huyo alisema siku hiyo, mumewe alirudi na kumuuliza walipo watoto wao wawili (hakuwataja majina) ambao aliwaondoa nyumbani siku kadhaa nyuma bila kumwambia.

Akasema, alipomuuliza hivyo tu, ndipo mumewe akamjia juu na kumshambulia kwa matusi huku akisema watoto aliwapeleka kuuzwa eneo linaloitwa Nyumba Ntobu. “Mume wangu alifika nyumbani, nilipomuuliza watoto wako wapi ndipo akanifungia ndani ya chumba na kunishambulia kwa matusi.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname