Binti wa miaka nane aitwaye Alani Santos kutoka mji wa San Gonzalo
nchini Brazil ameendelea kukusanya mamia ya watu kutoka sehemu
mbalimbali nchini kwake ambao hufika kanisani anakoabudu ambako baba
yake ni mchungaji ili waombewe na binti huyo anayeaminika kuwa na nguvu
za ajabu za kukemea mapepo na kuponya magonjwa akitumia jina la Yesu.
Katika mji anaotokea binti huyo unaweza kufananisha na Mbeya kwa hapa
Tanzania kutokana na kuwa na utitiri wa makanisa licha ya kwamba nchi
hiyo kwasasa inakabiriwa na tishio la watu kutopenda masuala ya kiimani
kwasasa. Brazil taifa ambalo linasifika kuwa la Kikristo wa kanisa la
Katoliki, limekuwa na vipaji mbalimbali kupitia watoto akiwemo kijana
Jotta A ambaye uwezo wake wa kuimba ni wa ajabu kiasi cha hata
kuwashangaza waimbaji wakubwa maarufu duniani.


No comments:
Post a Comment