27 March 2014

MASHABIKI WA MAN U WAELEKEZA HASIRA ZAO KWA MOYES NA ALEX FERGUSON

Shabiki akimtukana David Moyes

Kichapo cha bao 3-0 walichopata jana kutoka kwa Manchester City kimewakasirisha mashabiki wa Manchester United, na wameamua kuelekeza hasira zao kwa kocha Davidi Moyes na Sir Alex Ferguson.
Kufungwa huko kulipandisha hasira za mashabiki wa timu hiyo ambapo wale waliokuwa karibu na David Moyes walilazimika kushikwa na walinzi wakitaka kumshambulia huku wengine wakielekeza hasira zao kwa Ferguson.
Mashabiki wanalaumu uamuzi wa Ferguson kumwachia mikoba Moyes kama kocha wa Manchester United.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname