05 March 2014

ALIYEUA BAADA YA KUMFUMANIA MKEWE AAHUKUMIWA JELA MWAKA 1,KWA KUUA BILA KUKUSUDIA HUKO TABORA

Kijana Sanane Machimi akiwa mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi mkoa wa Tabora  muda mfupi baada ya kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja kufuatia kosa la mauaji ya bila kukusudia.Mahakama ya hakimu  mkazi  mfawidhi mkoa wa Tabora  imemuhukumu  kutumikia kifungo cha mwaka mmoja Jela  kijana anayefahamika kwa  jina la  Sanane Machimi baada ya kupatikana  na  hatia ya kuua bila kukusudia.

Akisoma  maelezo ya kosa mbele  ya mahakama hiyo,Mwanasheria upande wa Jamhuri  Bw.Nestory  Paschal  aliieleza mahakama hiyo kuwa mshtakiwa  Sanane Machimi akiwa na umri wa miaka  17 mnamo  tarehe  7 mwezi wa 5 mwaka  2012 alimuua bila kukusudia  mtu  mmoja aliyefahamika kwa jina la Kweji  Ntuvilo kwa kumpiga kwa fimbo kichwani na ubavuni  baada ya kumfumania  anafanya  mapenzi na mkewe  eneo la  vichakani  huko wilayani  Sikonge.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname