YANGA YAUA KAGERA, SHUJAA NGASSA NA KIIZA, SIMBA SC YAENDELEA KUNG'ARA KILELENI
YANGA SC imeshinda mchezo wa kwanza wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ugenini msimu huu baada ya kuilaza
Kagera Sugar mabao 2-1 Uwanja wa Kaitaba, Bukoba jioni hii, wakati
watani wao wa jadi, Simba SC pia wameshinda 1-0 dhidi ya Prisons Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam.
Jonas Mkude
Uwanja wa Taifa, bao pekee la Simba SC
limefungwa na Jonas Mkude dakika ya 62, wakati Uwanja wa Kaitaba, mabao
ya Yanga yamefungwa na Mrisho Ngassa dakika ya kwanza na Hamisi Kiiza
57, wakati la Kagera limefungwa na Godfrey Wambura dakika ya 47. Coasal
Union na Ashanti zimetoka 1-1 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es
Salaam. HABARI ZAIDI ITAFUATIA.
Ngassa akishangilia na Mbuyu Twite baada ya kufunga (
Chanzo:http:bongostaz.blogspot.com
No comments:
Post a Comment