17 October 2013

VIDEO: WANAFUNZI WA UDOM WA MWAKA WA KWANZA AMBAO NI RAIA WA MOZAMBIQUE WANATIA HURUMA........WAMWAGA MACHOZI,AMBASSADAR WA NMB WAPATA KAZI YA ZIADA:




Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma ambao Raia wa kigeni leo wamejikuta katika hali ya simanzi na majonzi baada ya kukutana na wenzao ambao wapo college tofauti , wanafunzi hao walijikuta wamekutanishwa kwa pamoja bila kutegemea  baada ya Ambassador wa NMB maarufu kama Team kicollege pluS  kuwakutanisha na kuwapa elimu juu ya huduma za NMB, ishu ilikuwa ni baadhi ya wanafunzi hao Raia wa kigeni  ambao wapo college ya social waliomba ambassador wa NMB kuwapeleka
wanafunzi hao ili waungane na wenzao ambao wapo college ya Tiba (medicine) na kupewa elimu juu ya huduma za NMB ila hali ilikuwa tofauti baada ya wanafunzi kuwaona wenzao kwanza hawakuamini na pili walijikuta katika hali ya kuangua kilio kwa madai ya kwamba wanafunzi wa kibongo wanawatenga na kuwanyanyapaa na  tena huwa wanajisikia vibaya kwa sababu ya kwamba wanahisi kunyanyapaliwa kwa sababu wapo nchi ambayo siyo yao..... kiukweli raia hao hawafamu lugha ya kiswahili na pia kingereza chenyewe ni cha magumashi lkn linapokuja swala la kuwatenga siyo ishu kabisa . Na walikuwa wanatia huruma sana kwa jinsi walivyokuwa wanaelezaa,Pia ambassadar wa NMB walijikuta katika kazi ya ziada ya kuwabembeleza na kutatua swala hilo kwa kuwaahidi kulipeleka kwa uongozi wa chuo hicho:TAZAMA VIDEO HAPO CHINI JINSI ILIVYOKUWA LEO HII CHUONI HAPO:
source-bossngasa

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname