15 November 2015

Kwa Mara ya Kwanza Wastara Aonyesha Miguu Yake na Kuandika Mazito

Kwa Mara ya Kwanza Wastara Aonyesha Miguu Yake na Kuandika Mazito
Kwa mara ya kwanza toka nimekatwa mguu miaka 6 iliyopita leo nimechukua nafasi hii kupost hii pic kuondoa maswali mengi yaliyopo vichwani mwa watu
Nipo kama unavyoiona pic
Huyo ndio wastara nilivyo hakuna kilichopungua zaidi ya hicho unachokiona
Kuwa mlemavu ni kitu kingine tofauti ukiwa mzima hivyo kusikia maumivu na kuumwa mguu ni kitu cha kawaida
Sasa nipo nairobi kimatibabu na tatizo ni operetion ya kwanza nilikosewa ndio sababu ya maumivu ya mara kwa mara madaktari wameshajua nini cha kunifanya ili kuondoa mateso kwangu
Jifunze kitu kupitia hii pic yangu na si kucoment ujinga jiulize ungekuwa wew mama yako dada yako mume,mke, wako ungeweza kusmile kma mimi hali ya kuwa una maumivu?
Jifunze kitu kupitia wastara
na sijajidharirisha nimetaka wewe unijue nilivyo ili usiteseke na maswali juu yangu
Sijakatwa miguu yote kma ilivyovumishwa na pia pamoja na maumivu ninaweza kutembea japo si mwendo mrefu sana na naendelea kusmile
SOTE TUSEME ALHMADULILAH
ASANTE MUNGU
Wastara Juma @wastara84 on instagram

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname