Ilianza
kama ishu ya kawaida hivi lakini muda ulivyozidi kwenda ikazidi
kuchukua headlines kwenye mitandao ya kijamii kwamba eti kuna watu
wananunua sarafu za shilingi mia tano za Tanzania alafu wanatumia madini
ya sarafu hiyo kutengeneza vito kama mikufu hivi !
Nimepitia
kwenye channel ya Youtube ya blogger mkubwa Tanzania, Issa Michuzi
>>>Michuzi TV na nimekutana na hii stori nikaona niisogeze hapa
kushare na wewe pia.
Anayehojiwa
ni Abdul M. Dollah ambaye ni Meneja Msaidizi wa Huduma za Kibenki Benki
Kuu TZ… Majibu yake ni haya kuhusu hiyo ishu; “Huu uvumi tumeusikia
wananchi wengi wanakuja na kuulizia habari hiyo, huo ni uvumi tu na sio
kweli kwamba kuna madini yoyote katika hii sarafu ya mia tano ambayo
yanaweza kutengeneza vito vya thamani” >>> Abdul M. Dollah
“Wakati
tunaizindua hii sarafu mwaka jana tuliwaambia kwamba humu ndani kuna
madini ya chuma kwa asilimia 94 na madini ya Nikel asilimia sita tu…
Benki Kuu inaamini kwamba Wananchi wanadanganywa” >>> Abdul M.
Dolla
No comments:
Post a Comment