Mchezaji Jonas Mkude wa Simba
SC tayari yupo Afrika Kusini kwa majaribio katika klabu ya Bidvest Wits
na taarifa zinasema amepokelewa vizuri na kuthaminiwa ipasavyo.
Mkude amefikia kwenye nyumba nzuri na kupiga picha pembeni ya magari ya maana.
Mkude ameendelea kuwaomba Watanzania wazidi kumwombea ili aweze kufuzu majaribio.
Mkude aliondoka akiwa na
Baraka zote za Klabu ya Simba, Rais wa Simba Evans Aveva alisema “Simba
inamtakia kila la kheri Mkude kwenye majaribio yake kwenye Klabu ya
Bidvest Wits huko Afrika Kusini na hili liwe fundisho kwa vijana wengine
kuendeleza vipaji ili waweze kucheza mpira kwenye ligi za Nchi nyingine
kubwa hivyo kukuza upeo na vipaji Zaidi katika soka”. Alisema taarifa
ya Simba.
Mkude alizaliwa Desemba 3, 1992
Kinondoni B na kuanza soka lake akiwa mlinda mlango hadi kuwa kiungo wa
kutegemewa. Aidha alianza elimu ya msingi mwaka 1998 katika shule ya
Hananasif na kumaliza mwaka 2005
No comments:
Post a Comment