20 May 2015

ROSE NDAUKA LAWAMANI KWA PICHA HIZI ALIZOWEKA MTANDAONI


 
Staa mrembo wa Bongo Movies, Rose Nduka ametupiwa lawama na baadhi ya mashabuki wake kwa kuweka picha mtandaoni akiwa amalazwa hospital na wao kudhani kweli kumbe yupo ‘ON SET’ ya movie mpya.
Hapo jana Rose ndauka alibandika picha hiyo hapo juu akiwa amelala kwenye kitanda ya hospital na kuandika “AAR Hospital” kitendo ambacho kiliwafanya mashabiki weke wengi kudhani kuwa Rose anamwa na kuanza kumpa pole na kumuombea dua apone haraka.



Baada ya masaa kadhaa kupita, Rose akaweka tena picha nyingine tena akiwa hospital na kuwapa pole wale wote waliodhani kuwa anaumwa na kumpa pole, kwani yeye yupo lokesheni wanatengeneza movies mpya chni ya kampuni yake ya Ndauka Entertainment.
“Ohooo poleni wote mliojua naumwa pia ahsanteni kwa mapenzi yenu na nawapenda pia…new movie from Ndauka Entertainment”- Rose aliandika.

Mara baada ya kunadika hivyo baadhi ya mashabiki wakaibuka na kumlaumu kwa nini hakuandika hapo mwanzo, huku wengine kuwataka mashabiki hao wawe wanauliza kama kweli au la.
“Wenye akili tuliuliza hyo movie au?sababu sio kila anayelia amefiwa. Wabongo acheni kukurupuka...muwe mnauliza kwanza”,-shabiki moja alikomenti.
Huku wengine wasema kuwa walijua kuwa anaigiza ila wakaogopa kukomenti
“Mie nilihisi tuu ila nikaogopa kucomment labda unaumwa kweli then watu waanze kunishambulia mhh nikagopa maana heshima ni kitu cha bure.twaisubiri kwa hamu,”shabiki mmoja alikomenti.
Mzee wa Ubuyu

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname