05 May 2015

Pacquiao Bingwa wa Watanzania wengi, Wadai Mayweather alibebwa

pacquao 
Na. Richard Bakana, Dar es salaam
0656-407-587.
Katika kuanza na kumalizia siku ya Jumapili ya Mei 2 (Jana) Dunia nzima ilisimama kwa muda kwa wapenda masumbwi ambapo kulikuwa na mpambano wa Kihistoria kati ya Floyd Mayweather kutoka nchini Marekani na Manny Pacquiao wa Uphillipino na mtanange huo kumalizika Mamrekani huyo kuibuka na ubingwa kwa pointi.
Shaffihdauda.com imepita Mtaani na kuachwa mdomo wazi na mashabiki ambao wengi wao wamempatia Ubingwa Pacquiao wakisema kuwa ndiye aliyestahili kwani alipiga ngumi nyingi, alishambulia mwanzo mwisho, huku wengine wakisema kuwa Mayweather alikuwa akikimbia na hakuonyesha mchezo wa kuvutia licha ya kushinda.mayweather
Abdul Juma mkazi wa Tegeta, amefunguka na kusema hivi “Mchezo nimeushuhudia toka mwanzo kwenye mapambano ya utangulizi maana sikulala kabisa nikisubiria kwa hamu kubwa, Kama mimi ningekuwa Refa au Jaji katika mpambano huo basi Pacquiao ndio angekuwa bingwa wangu, Kwanza alikuwa anajiamini vya kutosha, alionyesha mchezo kweli ambao mashabiki tulitegemea maana alikuwa anashambuli na kumuandama Mayweather muda wote, Kiukweli jamaa alitoa burudani nzuri sana na nilitoka ukumbini nikifurahia namna Pacquiao alivyokuwa anacheza, Mimi nadhani Pacquiao amenyimwa ubingwa kwasababu alikuwa ugenini, majaji wote walimpendelea mwenyeji tu, Bingwa wangu ni Pacquiao”
John Raphael wa Magomeni amesema kuwa “Ule usemi wa mcheza kwao hutunzwa jana ndio nilikubali unafanya kazi, Pacquiao am,ezurumiwa haki yake masikini, Hatakama majaji wamempatia Mayweather ambaye alikuwa anakimbia ulingoni mimi nasema Bingwa ni Pacquiao, Sawa wanasema kuwa Mayweather alikuwa anapiga ngumi za uhakika lakini Mphillipino anajua kupiga ngumi”.Pacquiao-The-Fight
Zainabu Juma amesema “Kwanza sikulala kabisa nikijua mpambano utakuwa saa kumi, Kam uamuzi ungekuwa unatolewa na mashabiki basi Mayweather asingekuwa bingwa kwa Ukumbi mzima ulikuwa unamshangilia Pacquiao kutokana na kasi aliyokuwa nayo ya kupiga ngumi nyingi, pia alimuandama sana mpinzani wake, Lakini sisi ni watazamaji tu Majaji wao ndio walikuwa wanajua ngumi sahihi inatakiwa ipigwe wapi ili kupata pointi ndio maana mwisho wa siku Mmarekani kaibuka Mshindi”
Mussa Ally ‘M’babe’ amesema “Kwanza kabisa hawajamaa wote wanajua kupiga ngumi, Pacquiao anakasi kubwa sana na alipokuwa akimfikia mpinzani wake alikuwa anapiga ngumi nyingi kitu ambacho mashabiki wengi walikuwa wanafurahia lakini mwenzake alikuwa anazikinga kwa kuficha uso ambao ndio sehemu yenye pointi, Ni kweli kutokana na namna Pacquiao alivyocheza toka mwanzo alistahili kushinda lakini majaji ndio walikuwa wanajua kitu sahihi, Mayweather sawa alikuwa anaonekana kumkimbia mpinzani wake lakini hiyo yote ilikuwa kujihami na kujilinda ambapo hapo hapo alikuwa akipata mwanya anapinga ngumi yenye uhakika na pointi”Mayweather-v-Pacquiao-The-Fight
Hawadhi Nasibbu “Toka lini kuku akawika ugenini bwana, Mayweather alishinda sababu yuko Nyumbani, hata waliokuwa wakimshangilia ni watu wake wa karibu, lakini ile mashine Pacquiao ilikuwa ikishangiliwa na kila mtu kutoka na uwezo wake na kasi na namna alivyokuwa akimkimbiza mpinzani wake”
James Laurent “Mayweather ndio bingwa hayo ni maneno tu ya watu, kwanza alikuwa anapiga ngumi kwa malengo sio sawa na Pacquiao ambaye alikuwa anajipigia tu bila kujua wapi ngumi inatakiwa kwenda,
Katika mchezo huo ulikuwa wa kuvutia na wakihistoria uliamuliwa na majaji ambapo walimpatia Mayweather ushindi wa pointi 116-112, 116-112, na 18-110 dhidi ya Pacquiao.may pac

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname