Kajala akiwa na mwanaye Paula
Kazi kwelikweli! Mkali wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja ‘K’
amefunguka kuwa kwa umri aliofikia mwanaye, Paula Paul wa miaka 14 ana
kibarua kigumu cha kuhakikisha anakuwa salama hasa kwenye suala la
wanaume.
Mtoto wa Kajala Masanja ‘K’, Paula Paul.
Akichezecha taya na Ijumaa Wikienda wikiendi iliyopita, Kajala alisema
kuwa kwa umri huo, Paula ambaye alizaa na Prodyuza wa Bongo Records,
Paul Matthysse ‘P Funky’ anahitaji uangalizi wa nguvu na kumsimamia kwa
kila jamabo ili kuwakwepa ‘mijitu mikware’ ambao wanaweza kumrubuni.
“Dunia ya sasa watu siyo wema kihivyo lakini naamini sitashindwa na Mungu anisimamie,” alisema Kajala.
No comments:
Post a Comment