15 April 2015

KAJALA: NINA KIBARUA KIGUMU KWA PAULA WANGU, HASA KUMLINDA NA WANAUME


Kajala akiwa na mwanaye Paula
Kazi kwelikweli! Mkali wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja ‘K’ amefunguka kuwa kwa umri aliofikia mwanaye, Paula Paul wa miaka 14 ana kibarua kigumu cha kuhakikisha anakuwa salama hasa kwenye suala la wanaume.
 
  Mtoto wa Kajala Masanja ‘K’, Paula Paul.
Akichezecha taya na Ijumaa Wikienda wikiendi iliyopita, Kajala alisema kuwa kwa umri huo, Paula ambaye alizaa na Prodyuza wa Bongo Records, Paul Matthysse ‘P Funky’ anahitaji uangalizi wa nguvu na kumsimamia kwa kila jamabo ili kuwakwepa ‘mijitu mikware’ ambao wanaweza kumrubuni.
“Dunia ya sasa watu siyo wema kihivyo lakini naamini sitashindwa na Mungu anisimamie,” alisema Kajala.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname