04 February 2015

TAARIFA KWA UMMA BENKI YA I&M YAZINDUA HUDUMA YA KWANZA YA MFUMO WA KIELEKTRONIKI YA MASAA 24 KATIKA JENGO LA VIVA TOWERS, POSTA JIJINI DAR ES SALAAM













Jumanne 03/02/2015: I&M Bank (T) Limited imeendelea kuonyesha muelekeo mzuri katika soko baada ya kuzindua huduma ya kwanza na ya kipekee ya ya kibenki ijulikanayo kama “Banking lounge” itakayokuwa ikifanya kazi kwa masaa 24 kwa siku saba, ndani ya ghorofa ya kwanza katika jengo la Viva Towers, moja kati ya maeneo muhimu jijini Dar es salaam. Tanzania.

Hili ni jaribio la kipekee kwa Benki hiyo, kutoa huduma mbalimbali za kibenki kama vile;-Mashine ya kubadilisha fedha za kigeni, mashine ya mfumo wa ATM ya kuweka na kutoa fedha, “Siku yoyote, muda wowote” ndani ya masaa 24 katika siku saba za wiki.

MASHINE YA KUBADILISHA FEDHA ZA KIGENI: Ni sehemu ya kubadilishia fedha itakayokuwa ikifanya kazi kwa muda wa masaa 24 ndani ya siku saba za wiki. Hii itamuwezesha mteja kubadilisha fedha zake za kigeni na kupokea shilingi ya kitanzania bila ya kuwa na mtoa huduma. Hii itakuwa na umuhimu zaidi kwa wateja ambao watapenda kufanya miamala yao hasa nyakati za jioni/usiku huku kukiwa hakuna haja ya mteja kuwa na akaunti ya benki hiyo pindi anapotaka kupata huduma hii bali anachohitaji ni pasipoti halali ili kupata huduma.

MASHINE YA KUWEKEA FEDHA: Itamsaidia mteja kupata huduma kwa masaa 24 ndani ya siku saba hasa kwa maduka na biashara yanayofungwa mida ya jioni/usikuili kuweka fedha za mauzo yao ya siku nzima katika akaunti za benki zao muda wowote. Huduma hii ni ya kila siku ikiwemo siku ya jumapili na siku za sikukuu. Benki hii imefunga “kifaa maalum cha kuwekea fedha”, ambacho kiasi chochote kikubwa cha fedha kinaweza wekwa kwa usalama wa hali ya juu katika mashine hiyo pasipo na uhitaji wa mtoa huduma wa benki.
Mashine hii itahesabu fedha na itatoa risiti kwa mteja. Mashine hii ina kasi ya ajabu na uwezo mkubwa wa kuweka fedha nyingi, ikiwa na teknolojia ya hali ya juu kama vile kitambua fedha endapo itakua ni feki au la, kichambuzi na kitambuzi namba n.k.
MASHINE ZA ATM: Mashine za ATM zilizowezeshwa na VISA zitakazokuwa zikifanya kazi kwa masaa 24 zitawahudumia wateja na wa watumiaji wa kadi za VISA.
Zaidi ya huduma hizi za hali ya juu, Benki pia imeanzaisha “VIP SERVICE LOUNGE” ambayo inatoa huduma ya kibenki isiyo ya fedha, katika hali ya kisasa na starehe. Ikiwa na TV na mashine za kujipatia kahawa, mteja anaweza kukaa na kupumzika, katika hali salama, wakati wahudumu waliofunzwa kwa umahiri wakiendelea kumhudumia, kuanzaia saa 2 asubuhi mpaka saa 2 usiku. Pia wahudumu watasikiliza na kupokea mahitaji yote ya wateja yatakayotolewa huduma katika tawi letu la Maktaba kama vile:-maombi ya kufunguliwa akaunti, maombi ya TT/TISS, huduma za vitabu vya hundi, kadi za malipo ya kabla ya fedha za kigeni, huduma ya kadi za ATM, mikopo, maombi ya kadi za BPesa, taarifa nyingine za kibenki na msaada katika huduma nyingine za kibenki.
I&M imekuwa ni benki ya kwanza kuanzisha huduma hii ya teknolojia ya hali ya juu katika soko la Tanzania ambapo “Smart Banking Solutions Ltd” kwa mara nyingine tena imepiga hatua kwa kuungana na benki hiyo na kufunga  mashine za kuweka na kutoa fedha sambamba na kubadilishia fedha za kigeni.” .

Akielezea faida za mfumo huu, Afisa mtendaji mkuu wa benki ya  I&M  Bw. Anurag Dureha alisema  “Kwa mfumo huu mpya mteja wa I&M sasa atakuwa na uwezo wa kutumia huduma za kibenki kwa urahisi”. Tawi hili jipya linampa mteja njia mbadala za kufanya miamala, zaidi ya ile ya awali kama vile matawi ya benki, intaneti na simu za mikononi.
“Kwa kuanza, fedha ya kigeni itakayobadilishwa na mashine hizi ni dola za kimarekani muda mfupi baadae tutaongeza fedha nyingine za kigeni ili kutimiza mahitaji ya wateja wetu wanaotoka sehemu mbalimbali duniani kote” aliongeza Bw. Dureha

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname